Ajuza aliyejaribu kutenganisha vita kati ya wanawe watatu agongwa vibaya hadi kifo, Kakamega

Muhtasari

•Makomere Shikokongo (35) , John Omoro  (25) na Joseph Amakobe (40) walikuwa wanapimana nguvu  nje ya nyumba ya mama yao katika kijiji cha Ibokolo, kaunti ya Kakamega kuhusiana na mzozo usiojulikana wakati msiba huo ulitokea.

crime scene 1
crime scene 1

Vita kati ya ndugu watatu iligeuka kuwa mauti baada ya mmoja wao kumgonga mama yao vibaya  alipojaribu kuwatenganisha na kumsababishia maumivu yaliyomwangamiza

Wakati vita kati yao ilikuwa imechacha, mama yao aliingilia kati  akikusudia kuwatenganisha ila mmoja wao , ambaye alitaka kitanzi kiendelee kutamba akamgonga na kumwangusha chini.

Mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 60 alianza kulalamika kuhusu maumivu mabaya mwilini ila hakuna aliyempeleka hospitali. Baaadae alipatikana akiwa amefariki ndani ya nyumba yake.

Kufuatia hayo  wapelelezi walimtia mbaroni mshukiwa mkuu, Makomere Shikokongo ambaye anatarajiwa kufikishwa mahakamani kujibu mashtaka ya mauaji.