- Kesho yake ,akitaka kujua iwapo ni ukweli kwamba mpenzi wake alikuwa pia akionana na babake ,jamaa huyo aliamua kwenda naye katika hoteli ile ile ili kuona iwapo kuna wahudumu watakaomjua .
- Vita hivyo vilivyodumu saa kadhaa huku kila mmoja kati ya baba na mtoto wake akitumi chochote alichopata mbele kumpigia mwenzake .Polisi ndio walioingia kati kuwaeka seli hadi kesho yake
Kahaba mmoja mrembo amewafanya mtu na babake kuzabana makofi na kurushiana makonde mazito mazito katika danguro moja vungani mwa ji wa Turbo.
Chanzo cha vita vyao ni kwamba kila mmoja kati yao anadaiwa kwamba mwanamke huyo ni mpenzi wake lakini wakaazi wanafahamu kwamba licha ya ‘kuwacheza’ kwa kuchuma kutoka nyungu zao wawili , mwanamke huyo pia ni kahaba na anafahamika sana kwa kutoka na wanaume wengi wanaofanya kazi za kuendesha matrela ya masafa marefu . Amewateka fikra mtu na babake kwa kiasi kwamba hakuna kati yao anayeamini kwamba mwanamke huyo huuza mwili wake ili kupewa pesa .
Masaibu yaliyopeleka vita kuzuka kati ya mtu na mwanawe yalianza siku ambayo rais Uhuru Kenyatta alitangaza kwamba muda wa kafyu sasa utazidishwa ili kuanza kutekelezwa saa tatu za usiku na sio saa moja . Hatua hiyo iliwafanya watu wengi kzuidisha shughuli zao hadi nyakati za usiku pasi na kuogopa viboko vya polisi ambavyo wengi walikuwa wanaogopa kuanzia saa moja . Siku huyo mwanamke huyo aliyetambuliwa kama Rebbeca alikuwa katika mkahawa mmoja na mwanamme ambaye wengi walijua kwamba Rebbeca alikuwa apia’akimhudumia’ babake katika eneo hilo .
Kesho yake ,akitaka kujua iwapo ni ukweli kwamba mpenzi wake alikuwa pia akionana na babake ,jamaa huyo aliamua kwenda naye katika hoteli ile ile ili kuona iwapo kuna wahudumu watakaomjua . kwa bahati mbaya ,mmoja wa wahudumu hao alipasua mbarika alipomuuliza yule mwanadada iwapo ni yeye alikuwepo pale ba ‘babake’ siku iliyotangulia . Hapo ndipo ndipo sarakasi zilipoanza , jamaa alianza kufoka akimshtumu babake kwa kutaka kuharibu uhusiano wae na Rebbeca na kwenda katika hadware ya mzee wake ili kumkabili kwa lengo la kumkomesha . mji wote ulisimama kushuhudia baba na mwanawe wakimpigania mwanamke Yule ambaye hakuna aliyekosa kumjua kwamba alikuwa kahaba katika sehemu hiyo .
Vita hivyo vilivyodumu saa kadhaa huku kila mmoja kati ya baba na mtoto wake akitumi chochote alichopata mbele kumpigia mwenzake .Polisi ndio walioingia kati kuwaeka seli hadi kesho yake .Rebbeca hajaonekana tangia hapo na wengi wanasema amezihamishia huduma zake hadi mjini Eldoret .