Msamaha wake unajiri siku moja baara ya rais Uhuru pia kuomba msamaha

Ruto aomba msamaha kwa niaba ya Serikali kuhusu ghasia za Nyamira,Murang’a

Ruto amesema ni muhimu kwa viongozi kuvumiliana

Muhtasari
  • Ruto asema vitoa machozi havifai kuwa na karibu na kanisa au waumini 
  • Asema viongozi wanafaa kuheshimiana   hata wanapotofautiana katika maoni 
  •  Kibwana amesema magavana hawafai kukubali kutishwa 

 

Naibu wa Rails William Ruto

 

 Naibu wa Rasi William Ruto amewataka viongozi kuwavumilia wenzao . Amesema   ni vyema iwapo viongozi wataheshimu maoni na misimamo ya wenzao  hata wanapotofautiana

 “ Tushirikiane . Tunataka nchi  ambayo sote  tunaweza kutembea pamoja’ amesema Ruto

 Alikuwa akizingumza siku ya jumapili katika kanisa la  AIC huko Bomani  ,Machakos

 Naibu wa rais alikuwa ameandamana na  gavana  wa   Makueni Kivutha Kibwana, wabunge Victor Munyaka (Machakos), Vincent Musyoka (Mwala), Nimrod Mbai (Kitui East), Aisha Jumwa (Malindi), Kimani Ichung’wa (Kikuyu), George Theuri (Embakasi West) na Nixon Korir (Lang’ata).

 Ruto aliomba msamaha kwa niaba ya serikali kuhusu  ghasia zilizoshuhudiwa katika  maeneo ya  Murang’a, Kakamega na Nyamira .

“ Hatufai kushuhudia mambo kama hayo katika nchi inayomtii mungu . vitoa machozi havifi kuwa karibu na kanisa au waumini’ amesema Ruto

 Akiunga mkono wito huo wa Ruto ,gavana Kivutha Kibwana amesema viongozi na hasa magavana  hawafai kukubali kutishwa kuchukua misimamo Fulani ya kisiasa .

 “ Tuliipigania katiba hii kwa sababu  tulijua itamchukulia kila mtu kuwa sawa.Hatujafurahi kuhusu jinsi mambo yanavyoendeshwa katika nchi hi’ amesema Kibwana

 Gavana huyo wa Makueni amesema katiba ya sasa haiheshimiwi