Kituyi kugombea urais 2022

Mukhisa Kituyi hatimaye atangaza kwamba atagombea urais 2022

Kituyi amekuwa katibu mkuu wa UNCTAND tangu septemba mwaka wa 2013 na aliwahi kuwa waziri wa biashara na viwanda kuanzia 2002 hadi 2007

Muhtasari
  • Mukhisa  aliongeza , "  Watu  hawafai kutuambia mbona wanataka kuwa rais bali wanafaa kutuambia  sababu za kutaka uongozi’
  • Kituyi amesema anakamilisha muda wake kama mkuu wa UNCTAD   na atarejea nchini kwa kampeini   kabambe za kuingia Ikulu .
Waziri wa Ugatuzi Euge Wamalwa akiwa na mkuu wa UNCTAD Mukhisa Kituyi

 Mkuu wa shirika la UNCTAD   Mukhisa Kituyi ametangaza kwamba atawania urais mwaka wa 2022

 Akizungumza katika ngome yake ya Bungoma siku ya jumamosi baada ya kukutana na  kundi la watalaam kutoka eneo hilo  Kituyi amesema  analenga kuwania kiti hicho kwa sababu taifa kwa sasa lina ‘pengo la uongozi’ kwa ajili ya jitihada za kumriti trais Uhuru Kenyatta mabaye muhula wake wa pili utakaribia kufika tamati .

 “ Kila changamoto ni fursa kwetu …changamoto kwetu ni kwamba tuna  idadi kubwa ya watu bila uongozi na ni wakati wetu kuongoza’ amesema

Mukhisa  aliongeza , "  Watu  hawafai kutuambia mbona wanataka kuwa rais bali wanafaa kutuambia  sababu za kutaka uongozi’

Kituyi amesema anakamilisha muda wake kama mkuu wa UNCTAD   na atarejea nchini kwa kampeini   kabambe za kuingia Ikulu .

 Kuhusu uongozi wa jamii ya  Waluhya  Kituyi amesemajamii hiyo  haijakuwa kiongozi  kwa muda mrefu  na  ndio kwa sababu viongozi wengi wamejaribu kuleta umoja wa jamii hiyo bila mafanikio .

 Kituyi amekuwa katibu mkuu wa UNCTAND   tangu septemba mwaka wa 2013 na aliwahi kuwa waziri wa biashara na viwanda kuanzia 2002 hadi 2007

 Awali alihudumu kama mbunge wa Kimilili kabla ya kupoteza kiti hicho kwa mbunge  wa sasa wa Tongaren Eseli Simiyu  baada ya eneo bunge la kimilili kugawanywa mwaka wa 2007 .