Sakata ya Sonko na Kibicho

Mike Sonko aagizwa kufika polisi kuhusu madai ya kuchomwa magari

Sonko anafaa kujiwasilisha kwa maafgisa wa DCI katika makao makuu ya idara hiyo jumatatu ijayo

Muhtasari
  • Sonko  alidai kwamba  yeye ,Kibicho na maafisa wengine serikalini walinunua magari na kuyachoma  mwaka wa 2017 na kisha kukilaumu chama cha ODM  kwa ghasia hizo.
  •  Alizungumza katika eneo la Dagoretti  katika hafla ambayo naibu wa rais William Ruto alihudhuria
Gavana wa zamani wa Nairobi Mike Sonko

  Polisi wamemuagiza gavana wa zamani wa  Nairobi ajiwasilishe  ili kuhojiwa kuhusu madai yake kwamba yeye na maafisa wengine wa serikali  walipanga na kutekeleza ghasia wakati wa uchaguzi mwaka wa 2017 .

 Sonko anafaa kujiwasilisha kwa maafgisa wa DCI katika makao makuu ya idara hiyo  jumatatu ijayo  . Agizo hilo kwa Sonko limetolewa na mkuu wa uhalifu mkuu Obadia Kuria . Hii ni baada ya katibu wa kudumu wa wizara ya usalama wa ndani Karanja Kibicho  kulalamika kwa polisi  kwamba Sonko alikiri kutekeleza uhalifu na anafaa kuchukuliwa hatua .

Sonko  alidai kwamba  yeye ,Kibicho na maafisa wengine serikalini walinunua magari na kuyachoma  mwaka wa 2017 na kisha kukilaumu chama cha ODM  kwa ghasia hizo.

 Alizungumza katika eneo la Dagoretti  katika hafla ambayo naibu wa rais William Ruto alihudhuria . Kibicho amekana madai hayo na kupa kuhakikisha kwamba Sonko analipia kwa uhalifu aliotekeleza .

Kibicho  alijondoa lawamani kuhusu madai hayo  na kumshtumu Sonko kwa kumchafulia jina .  Kibicho pia amesema atatafuta usaidizi wa kisheria na mahakama kuhusu  madai aliotoa Sonko ya kumhusisha na kifo cha  aliyekuwa makamu wa rais  marehemu George Saitoti .

Sonko amedai kwamba kuna njama ya kumuua yeye pamoja na naibu wa rais William Ruto  . Kibicho amewaambia polisi kwamba hatua ya Sonko kutoa madai hayo ni  kukiri kufanya uhalifu  na amesema atamshtaki Sonko kwa kumharibia jina.