- Igathe alikuwa akijibu kesi ambayo mpiga kura mmoja Patrick Kiiru amewasilisha kesi mahakamai kupinga uchaguzi mdogo Nairobi uliofaa kuandaliwa februari tarehe 18 .
- Kiiru amesema tume ya uchaguzi nchini IEBC haina mamlaka ya kuitisha uchaguzi kuziba nafai ya gavana hasa wakati ambapo kuna naibu wa gavana anayefa kuiziba nafasi hiyo .
Kizungumkuti sasa kimeibuka kuhusu siasa za kumrithi Mike Sonko katika jiji la Nairobi baada ya naibu gavana wa zamani Plycarp Igathe kuzuka na madai kwamba hatua yake ya kujiuzulu kutoka nafasi hiyo haikuwahio kufanywa kuwa rasmi na aaitaka mahakama kuingilia kati na kuamua Iwapo kweli kujizulu kwake kulitamatishwa kwa mujibu wa sheria .
Akikubali kwamba alijiuzulu januari mwaka wa 2018 Igathe amesema hatua ya kaunti kukosa kutambua kuondoka kwake afisini inamaanisha kwamba mahakama sasa inafaa kutoa usemi wake kuhusu hatua hiyo .
Kupitia wasilisho maalum kwa mahakama Igathe amesema kujiuzulu kwake hakukutambuliwa na spika wa bunge la kaunti . wasilisho hilo lilitolewa tarehe 12 januari na lilifichuliwa siku ya jumatano .
“ Ukosefu wa kufuata sheria katika kutambua kujiuzulu kwangu na hatua ya idara za kaunti kukosa kuchukua hatua za kufanya rasmi uamuzi wangu kuondoka kunamaanisha sasa kwamba hatima ya uamuzi wangu ipo mikononi mwa mahakama’ amesema Igathe .
Igathe alikuwa akijibu kesi ambayo mpiga kura mmoja Patrick Kiiru amewasilisha kesi mahakamai kupinga uchaguzi mdogo Nairobi uliofaa kuandaliwa februari tarehe 18 .
Kiiru amesema tume ya uchaguzi nchini IEBC haina mamlaka ya kuitisha uchaguzi kuziba nafai ya gavana hasa wakati ambapo kuna naibu wa gavana anayefa kuiziba nafasi hiyo .
Uchaguzi mdogo utabadilisha mkondo wa siasa jijini kwani utamaanisha kwamba wanaoshikilia naasi hizo watafanya hivyo kwa muda mfupi . Mpiga kura huyo amesema Igathe ndiye anauefaa kuchukua usukani kama gavana wa jiji la Nairobi .Kesi hiyo itasikizwa jumatano na jaji Weldon Korir .