- M.A alihukumiwa na hakimu mkuu Esther Boke baada ya mwendesha mashtaka Nancy Kerubo kumsomea mashtaka na ushahidi wa hatia yake .
- Mtuhumiwa polisi wamesema alimkojolea mtoto katika sehemu zake za siri januari tarehe 27 katika mtaa wa mabanda wa Deep Sea ,Kibra
Mwanamme mwenye umri wa miaka 56 amehukumiwa kifungo cha miaka mine jela baada ya kukiri shtaka la kumfanyia mtoto mwenye umri wa miaka 3 kitendo kisicho cha kawaida .
M.A alihukumiwa na hakimu mkuu Esther Boke baada ya mwendesha mashtaka Nancy Kerubo kumsomea mashtaka na ushahidi wa hatia yake .
Mtuhumiwa polisi wamesema alimkojolea mtoto katika sehemu zake za siri januari tarehe 27 katika mtaa wa mabanda wa Deep Sea ,Kibra
Kulingana na stakabadhi ya mashtaka mtoto huyo alikuwa ameachwa na mamake kwa jirani yao na baadaye akaonekana na jirani mwingine akiingia katika nyumba ya mshukiwa . Tukio hilo liliripotiwa kwa majirani wengine waliotaka kujua kilichokuwa kikifanyika na baadaye mshukiwa alionekana kuwashambulia majirani waliotaka kujua Iwapo mtoto huyo alidhulumiwa kwa njia yoyote .
“ Walipofkika katika mlango wa mshukiwa walimpata mtoto akiwa amebeba suruali yake ya ndani na alipohojiwa alisema mtuhumiwa alikuwa amemkojelea katika sehemu za utupu’
Hakimu amesema mtuhumiwa ana muda wa siku 14 kukata rufaa dhidi ya hukumu aliopewa .