Omar Lali alitumia 'uchawi' kumtongoza Tecra - Mahakama yaambiwa

Muhtasari

″James Karanja alisema Omar alijaribu kumtenga Tecra kutoka kwa familia yake na hakuta kujumuika nao.

  ″Marehemu Tecra alimwambia kuwa uhusiano wake na Omar Lali haukuwa wa kawaida lakini wa kiroho.

James Mavharia kakake maremu Tecra
James Mavharia kakake maremu Tecra

Ndugu wa mrithi wa Keroche Tecra Mungai siku ya Alhamisi aliambia mahakama mjini Nairobi kwamba marehemu Tecra alimwambia kuwa uhusiano wake na Omar Lali haukuwa wa kawaida lakini wa kiroho.

James Karanja alisema Omar alijaribu kumtenga Tecra kutoka kwa familia yake na hakuta kujumuika nao.

Msaidizi wa nyumbani wa Tecra alisema wawili hao walipigana mara kwa mara walipokuwa wakiishi Naivasha na Tecra alimwambia kwamba alimpiga usiku.

Mpenzi wa Karanja, Victoria Marcella, alisema Tecra alimwambia alimchukulia Omar kama nabii.

James Karanja, ambaye ni mtoto wa kwanza wa afisa mkuu mtendaji wa Kampuni ya vileo ya Keroche Tabitha Karanja, alisema kuwa mara nyingi Tecra alisema "sio uhusiano wa kawaida kati yake na Omar kwani ulikuwa wa kiroho na wa kupendeza zaidi."

Karanja aliongeza kuwa alipokwenda Lamu na mpenzi wake, alikutana na Tecra na rafiki yake Yvonne ambaye alimwambia kuwa Omar anatumia uchawi kutongoza wanawake.

Alikuwa akitoa ushuhuda katika uchunguzi wa kifo cha Tecra ambaye alikufa mnamo Mei 2, 2020 katika Hospitali ya Nairobi.

Inasemekana alikuwa ameanguka chini ya ngazi kubwa kwenye nyumba moja huko Lamu.

Alikutana na Omar kwa mara ya kwanza nchini Tanzania mnamo Agosti 30, 2019, wakati alikuwa ameenda kwenye sherehe ya kuzaliwa huko Dar es Saalam.

Mshukiwa Omar Lali
Mshukiwa Omar Lali

Alishtuka sana kuhusu uhusiano huo kwa sababu alijua marafiki wa zamani wa Tecra, lakini uhusiano na Lali ulimshangaza sana. Kulikuwa na kitu kisicho kawaida.

Lali alikuwa na umri wa miaka 30 zaidi ya umri wa Tecra. Mtindo wake wa maisha pia ulikuwa mbali na ule wa Tecra ikilinganishwa na mahusiano ya dada ya awali.

Sherehe ya siku ya kuzaliwa, alinishtua kwani hakutaka kukaa na familia. Alikuwa mbali nasi, ”korti iliambiwa.

"Tulikutana tena Novemba 8, 2019. Nilikuwa nimeenda kumtembelea alikokuwa mjini Lamu. Nilienda na rafiki yangu wa kike. Siku ya pili, Tecra alikuja mahali nilikuwa nikikaa, katika hoteli, na akaja na rafiki yake Yvonne. Yvonne alikuwa akifahamiana na Omar kwa sababu wote walikuwa kutoka Lamu, "alisema.

 

Wakati Tecra alipoondoka, alifanya mazungumzo ya haraka na Yvonne. Alimwambia anamjua Lali vizuri kwa sababu wote wawili walikuwa wakiishi Lamu.

"Alishauri kwamba Tecra amwache," korti iliambiwa.