•Kulingana na mashahidi, genge la majambazi watatu lilishambulia polisi wawili waliokuwa wameshika doria katika benki hilo, wakawapokonya bunduki zao na kuingia ndani ya benki
•Uvamizi huo unasemekana kuchukua muda wa dakika 10 kabla ya majambazi hao kuweza kutoroka kwa gari licha ya kukimbizwa na polisi.
Habari na Cyrus Ombati
Polisi upande wa Machakos wanawinda genge la majambazi walioiba bunduki za polisi na kuvamia benki ya Equity katika mji wa Matuu.
Kulingana na mashahidi, genge la majambazi watatu lilishambulia polisi wawili waliokuwa wameshika doria katika benki hilo, wakawapokonya bunduki zao na kuingia ndani ya benki.
Pale ndani ya benki waliamurisha wafanyakazi na wateja kulala chini kabla ya kufanya shughuli zao na kutoka.
Polisi walidai kuwa majambazi hao pia walishambulia maafisa waliofika kwenye eneo la tukio kwa risasi na wanashuku kuwa mmoja wao alijeruhiwa kwenye harakati hiyo.
Uvamizi huo unasemekana kuchukua muda wa dakika 10 kabla ya majambazi hao kuweza kutoroka kwa gari licha ya kukimbizwa na polisi.
Polisi waliendelea kuwafuata majambazi hao kwenye barabara kuu ya kuelekea Nairobi huku vizuizi vya barabara vikiwekwa kwenye maeneo mbalimbali.
Inadaiwa kuwa baada ya hatua kadhaa genge hilo lilibadilisha chombo chao cha usafiri na kuchukua pikipiki