Wanafunzi watatu wa shule ya msingi wafa maji Murang'a

Muhtasari

•Watatu hao walikuwa  wanaelekea nyumbani baada ya kunyolewa  walipoamua kuogelea kidogo.

Crime scene photo
Crime scene photo

Biwi la simanzi limetanda katika eneo la Gatanga, kaunti ya Murang'a baada ya wavulana watatu kufa maji walipokuwa wanaogelea mtoni Kiama siku ya Jumapili.

Watatu hao walikuwa  wanaelekea nyumbani baada ya kunyolewa nywele katika kinyozi kimoja mtaani Kirwara  walipoamua kuogelea kidogo.

Wapiga mbizi kutoka eneo hilo waliweza kutoa miili ya wavulana wawili jioni ya Jumapili huku mwili mmoja uliosalia ukitolewa Jumatatu asubuhi.

Wavulana hao walikuwa wanafunzi wa darasa la saba katika shule ya msingi ya Mabae iliyo eneo la Gatanga.