Harmonize akanusha madai ya kutuma watu kwa mahasimu wake

Muhtasari
  • Harmonize akanusha madai ya kutuma watu kwa mahasimu wake
Harmonize
Harmonize
Image: Hisani

Mwanamuziki wa Tanzania Harmonize amejitokeza wazi na kueleza hajawai tuma watu kuzungumza vibaya kuhusu washindani wake.

Harmonize almaarufu Konde  amefunguka haya kwenye kituo kimoja cha radio ambapo alieleza kuwa  haweza kumtuma mtu yeyote kuwasambulia mahasidi wake kwa sababu hakuna kitu chochote wataongeza kwa kazi zake.

Ikimbukwe ni mwaka jana ambapo  alifunguka kuhusu kilichomfanya kutoka katika lebo ya Wasafi iliyofanya ajulikane kimuziki. 

Ambapo alieleza aliyokumbana nayo hasa kwenye kipindi hicho alichokuwa akifanya kazi na lebo ya Wasafi inayomilikiwa na Msanii Diamond Platinumz.

Konde  alisema hayo baada ya kuulizwa  na mwanahabari kama huwa anawatuma watu kuzungumza vibaya kwa  mahasimu wake.

"Mkiona mtu yeyote anaenda kumzungumzia mtu fulani  basi ujue ni maamuzi yake na mimi binafsi siwezi kumtuma mtu yeyote   kwa  sababu hanisaidii." 

Alichukua nafasi hio kupiga vijembe wanaoongea vibaya  kuhusu Kikundi chake cha  Konde Gang akitaja kuwa wanakiogopa kwa sababu kimeanza kuonyesha ni jinsi gani kinaweza leta ushindani kwenye muziki. 

"Ukiona mtu anatuma watu wamzungumzie mtu fulani, basi ujue anawaza kukuhusu"  Alisema  Harmonize