•Todd amejitokeza na kuomba msamaha kufuatia video yenye ilikuwa ikienea kwenye mitandao ya kijamii akiwa kwenye madhabau.
•Alieleza kwamba ingawa Yesu aliweza kutumia mate yake kutenda mijiuza, kwa kipindi hiki hasa cha Corona alikosea kutumia mfano aliotumia kwenye video hio,
Mhubiri Mike Todd ameomba msamaha kufuatia video ilikuwa ikitamba kwenye mitandao ya kijamii akiwa kwenye madhabahu.
Kwenye video hio, Mhubiri huyo alionekana kwenye madhabau akitema mate kwenye kiganja cha mkono kisha kumpaka mshirika.
Todd alisema kwamba alikuwa anatumia tukio hilo kama mfano lakini alikuja kufahamu kwamba alikuwa amevuka mipaka katika mfano wake.
Alieleza kwamba ingawa Yesu alitumia mate yake kutenda miujiza, kwa kipindi hiki hasa cha Corona alikiri kuwa mfano aliotumia kwenye video hiyo haukufaa, huku akikiri ameelewa bayana madhara ya kutumia mfano huo na kuwaeleza washirika wake kwamba tukio hilo limekuwa funzo kwake na wachungaji wengine.
Kulingana naye tukio hilo ni la kusambaratisha ujumbe huo na kusema wakati ujao atatafakari upya mifano atayokuwa anatumia katika mahubiri yake.