• Nandy amekuwa hivi majuzi akionekana akivaa nguo kubwa kubwa kitu ambacho si kawaida yake huku mashabiki wakitabiri kuwa msanii huyo ana ujauzito.
• Kwenye video hiyo, ambayo Mwijaku alichapisha kwenye ukurasa wake wa Instagram alionekana akishika malkia huyo tumbo lake na kuthibitisha kuwa hana ujauzito wowote.
Baada ya uvumi kuenea kwenye mitandao ya kijamii kwamba msanii wa Bongo Flava Nandy almaarufu The Afican Princess kwamba ana ujauzito.
Wandani wake hasa Mwijaku wamejitokeza na kutupilia mbali madai hayo.
Nandy amekuwa hivi majuzi akionekana akivaa nguo kubwa kubwa kitu ambacho si kawaida yake huku mashabiki wakitabiri kuwa msanii huyo ana ujauzito.
Mwijaku alitumia kipindi ambacho msanii huyo alikuwa amealikwa kwenye kituo kimoja cha habari nchini Tanzania, kuweka bayana mambo kwa kupuuzilia mbali madai kwamba Nandy anatarajia kufungua na kuwaonya wanaoeneza uvumi huo kukoma.
Kwenye video hiyo, ambayo Mwijaku alichapisha kwenye ukurasa wake wa Instagram alionekana akishika malkia huyo tumbo lake na kuthibitisha kuwa hana ujauzito wowote.
"Na jambo nzuri zaidi Nandy si mjamzito, watu mliosema Nandy ni mjamzito hapana, nimemguza kwa mkono wangu mimi, hana...ndugu yangu Bilyass unakwama wapi?" Mwijaku alisema kwenye video hiyo.