•Msanii wa kike Vanessa Mdee amefunguka kuhusu mahusiano yake na mume wake, Rotimi huku akibaini ndiye alifanya habadilishe msimamo wake na kuwa mama
Msanii wa kike Vanessa Mdee amefunguka kuhusu mahusiano yake na mume wake, Rotimi huku akibaini ndiye alifanya abadilishe msimamo wake na kuwa mama.
Wawili hao ambao wamefungua app ya burudani wamekuwa kwenye mahusiano kwa takribani mwaka mmoja.
Kulingana na Vanessa, mambo ya kuwa mzazi hayakuwa kuwa kwenye akili yake kitambo lakini aliomba watu wasije wakatafsiri kauli hiyo vibaya.
"Mnafaa kuelewa, kwa sababu kama mlikuwa mnanijua kitambo sikuwahi kuwa na mipango ya kuwa mama, hata sikuwa nafikiria kuwa mama ila mtazamo wangu ulibadilika wakati nilikutana na mpenzi wangu Rotimi ambaye alifanya nibadilishe mawazi yangu na kumzalia mtoto mmoja basi nikakubali, lakini msinielewe vibaya kuwa napenda watoto," alisema Vanessa.
Vanessa ni mama wa mtoto mmoja kwa sasa anafurahia maisha ya kuwa kwenye ndoa. Ni mwaka jana ambapo alieleza kuacha kuimba kwa muda huku akieleza masaibu ya wanamuziki.