•Aliwapongeza mashabiki wake kwa kuonyesha upendo wakati wote huo ambao amekuwa kwenye tasnia ya uigizaji
•Alieleza kuwa kuchanga kwa mashabiki wake kulionyesha jinsi Watanzania wanamdhamini Muigizaji
Muigizaji wa Filamu za Bongo Wema Sepetu ameeleza kuwa hajawai kumwambia mtu yeyote kumfanyia mchango ili anunue gari.
Muigizaji huyo hata hivyo alisema kwamba waliomchangia walifanya hivyo kwa hiari yao wenyewe.
Akihojiwa kwenye kituo kimoja cha habari nchini humo, Sepetu alisema kuwa kuchanga kwa mashabiki wake kulionyesha jinsi Watanzania wanamdhamini.
"Mimi binafsi sikuwai kuomba mtu yeyote anichangie pesa, nadhani ilikuwa kuonyesha jinsi wanavyonipenda na watu wakaamua wafanye walichokuwa wakifanya lakini nilishawambia kwamba sipendi na wasitishe michango. Na nina imani walisitisha, kusema ukweli sijui kilichoendelea kutoka hapo na sikutaka kujihusisha kwa sababu sijawai kutoka mwanzo kuomba pesa,"alisema Wema Sepetu.
Kauli ya Wema imejiri baada ya kuwa kimya kutokana na maneno aliyoyasema Aristostle kwamba ni muigizaji mashuhuri ambaye hana gari la kifahari kama waigizaji wengine.
Hata hivyo alikwepa kuzungumzia kauli hiyo,huku akitaja kuwa Aristostle alikuwa na nia mbaya ya kumdhalilisha kwa hivyo haikuwa na haja ya kujadili kauli yake.
Vilevile aliwapongeza mashabiki wake kwa kuonyesha upendo wakati wote huo ambao amekuwa kwenye tasnia ya uigizaji.