Uhasama wa Raila na Ruto wanoga

Hizi kauli za Ruto zitaitumbukiza Kenya mashakani-Raila

Raila amedai pesa wanazopewa wakenya sasa zilifujwa kutoka serikalini

Muhtasari
  •  Raila hata hivyo amesema hatua hiyo ni bomu la muda  na haifai kuruhusiwa kuendelea .
  •  Amewarai vijana kuunga mkono ripoti ya BBI  kwani ina mapendekezo ya kushughulikia matatizo kama vile ukoefu wa ajira na kuwapa fursa nyingi za kujiendeleza .

 

Naibu wa rais William Ruto na kiongozi wa ODM Raila Odinga

Kiongozi wa ODM Raila Odinga  amesema kwamba matamshi anayotoa naibu wa rai William Ruto yanaitia nchi katika hatari ya kugawanyika na kusababisha umwagikaji wa damu . Odinga amesema kauli za Ruto zinajenga uhasama wa matabaka a kwa kuendeleza siasa za kuwatenganisha wanaodaiwa kuwa navyo na wasio navyo .

 Raila amekemea usemi wa siasa za Ruto  wa makabiliano kati ya Dynasty na Mahasla  akiema kwamba  mkondo huo  ‘unahatarisha  uthabiti na  amani ya nchi yetu’.

 Ruto amezitega siasa zake za kuwania urais kwa msingi wa  kuwatetea mahasla  wasio navyo dhidi ya wanasiasa wanaodaiwa kuwa na mali na kutoka familia tajika kisiasa . Vugu vugu la mahasla  limeonekana kuipa wasi wasi serikali kwani  usemi huo unazidi kushika kasi na kutawala mijadala kuhusu siaa za kumrithi rais Uhuru Kenyatta mwaka ujao .

 

 Raila hata hivyo amesema hatua hiyo ni bomu la muda  na haifai kuruhusiwa kuendelea .

 Alitoa  mfano wa  kiongozi wa zamani wa Ujerumani Adof Hitler  ambaye aliendeleza kampeini ya kuwachochea wajerumani dhidi ya wayahudi  na baadaye kulitumbukiza bara ulaya katika kipindi cha umwagikaji wa damu na vita .

 Kinara huyo wa ODM  amesema kauli za Hitler katika miaka 1930 ziliipeleka ujerumani  nusra isambaratike kwa kuendeleza uhasama dhidi ya wayahudi

Raila  ameonya kuhusu kuendelezwa kwa siasa za mahsla  akisema Iwapo hazitakomeshwa basi Kenya huenda ikajipata katika nafasi ya Ujerumani miaka  ya 1930’s

 Amewarai vijana kuunga mkono ripoti ya BBI  kwani ina mapendekezo ya kushughulikia matatizo kama vile ukoefu wa ajira na kuwapa fursa nyingi za kujiendeleza .

 “ Ndio kwa sababu tulianzisha BBI ,stakabadi  ambayo msingi wake ni kubadilisha  hali ya kijamii na kiuchumi ya taifa letu’ amesema Oinga .

 Raila alikuwa ameandamana na seneta wa Siaya  James Orengo, wabunge Esther Passaris (Nairobi), Abdulswamad Nassir (Mvita), Mishi Mboko (Likoni), Babu Owino (Embakasi East)  na mafanyibiashara  Agnes Kagure.

 

Raila  pia alitilia  doa mali ambayo Ruto anaitumia kuendeleza mradi wake wa mahasla  wakati ambapo serikali inazongwangwa na visa vingi vya wizi wa fedha za umma na ufisadi .

Amedai kwamba mradi wa SGR uliokuwa wa serikali ya muungano uliongezwa gharama  na serikali ya jubilee  kutoka shilingi bilioni 227 hadi shilingi bilioni 380 .

Amedai kwamba fedha zilizofujwa katika mradi huo ndizo zinaokabidhiwa wakenya wasiofahamu kinachofanyika .