•Tangazo hilo limetokana na video inayozunguka mitandaoni ikimuonyesha Raphael Tuju akitangaza kupokea barua ya kujiuzulu kutoka kwake Murathe.
•"Bwana Murathe anabaki kuwa naibu mwenyekiti wetu na anaendelea kutekeleza majukumu yake katika nafasi hiyo kwa bidii ili kutimiza majukumu yake kama ilivyoandikwa kwenye katiba ya chama" Jubilee ilitangaza.
Chama tawala cha Jubilee kimekanusha madai kuwa naibu mwenyekiti, David Murathe amejiuzulu kutoka uongozi wa chama hicho.
Tangazo hilo limetokana na video inayozunguka mitandaoni ikimuonyesha katibu mkuu wa chama hicho, Raphael Tuju akitangaza kupokea barua ya kujiuzulu kutoka kwake Murathe.
Tangazo hilo lilitolewa kupitia ujumbe ulioandikwa na mkurugenzi wa mawasiliano pale, Albert Memusi na kuwekwa kwenye kurasa rasmi za mitandao ya kijamii ya chama hicho jioni ya Jumanne.
"Bwana Murathe anabaki kuwa naibu mwenyekiti wetu na anaendelea kutekeleza majukumu yake katika nafasi hiyo kwa bidii ili kutimiza majukumu yake kama ilivyoandikwa kwenye katiba ya chama" Jubilee ilitangaza.
STATEMENT BY THE JUBILEE PARTY ON THE ALLEGED RESIGNATION OF THE JUBILEE PARTY VICE CHAIR, HON. DAVID MURATHE. pic.twitter.com/Amg3WXUpVI
— JUBILEE PARTY® (@JubileePartyK) May 26, 2021
Chama hicho kimesihi uma kutupilia mbali ripoti zinazosema kuwa Murathe aliacha kazi yake. Kimesisisitiza kuwa matangazo rasmi yatatolewa kupitia njia rasmi ila si uvumi tu.
"Mawasiliano rasmi kuhusu mabadiliko katika chama yatazungumzwa kupitia njia rasmi kama ilivyo kawaida na kama ilivyoandikwa kwenye katiba ya chama" Memusi aliandika.
Chama hicho kinachoongozwa na Rais Uhuru Kenyatta kimekuwa kikikumbwa na misukosuko mingi ya kisiasa haswa baada ya kupoteza viti zote katika chaguzi ndogo zilizofanyika hivi majuzi.
David Murathe has resigned as Jubilee Party Vice Chair Raphael Tuju confirms.. pic.twitter.com/5NiHYZX0c3
— Trending in kenya (@Trendingken) May 26, 2021
Baadhi ya viongozi wamekuwa wakiwanyooshea kidole cha lamama David Murathe na waziri Fred Matiang'i huku wakiwaagiza kujiuzulu ikiwemo Ngunjiri wambugu wa Nyeri.