Mwili wa Charles Njonjo wachomwa katika maziara ya Kariokor

Muhtasari

•Hafla ya kuchoma mwili wa Njonjo ilifanyika takriban masaa matano baada yake kuaga dunia  alfajiri ya Jumapili akiwa nyumbani kwake Muthaiga.

Mwili wa Chrales Njonjo wachomwa katika chumba cha kuchoma maiti cha Kariokor
Mwili wa Chrales Njonjo wachomwa katika chumba cha kuchoma maiti cha Kariokor
Image: GORDON OSEN

Habari na Gordon Osen

Mwili wa Mwanasheria  Mkuu wa kwanza wa Kenya baada ya uhuru Charles Mugane Njonjo umechomwa katika chumba cha kuchomea maiti cha Kariokor.

Hafla ya kuchoma mwili wa Njonjo ilifanyika takriban masaa matano baada ya waziri huyo wa zamani wa Sheria na masuala  ya Katiba kuaga dunia  alfajiri ya Jumapili akiwa nyumbani kwake Muthaiga.

Hafla ya kumpungia Njonjo mkono ilihudhuriwa na wanafamilia wachache wa karibu.

Mwili wa Njonjo uliwasili katika chumba cha kuchomea maiti la Kariokor mwendo wa  saa tatu unusu asubuhi ukisindikizwa na takriban wanafamilia 25.

Hafla ya kuchoma mwili wa marehemu ilianza kwa ibada fupi ya familia. Waandishi wa habari na watu waasio wa familia hawakuruhusiwa kuingia.

Njonjo aliaga dunia mwendo wa saa kumi na moja asubuhi ya Jumapili, Januari 1, 2022.

Marehemu ambaye alitambulika sana kama 'The Duke of Kabeteshire' alifariki akiwa na umri wa miaka 101.

Rais Uhuru Kenyatta  amesherehekea marehemu kwa jukumu kubwa alilocheza katika ujenzi wa taifa  na kwa kazi nzuri aliyofanya kwa kujitolea alipofanywa mwanasheria mkuu wa kwanza baada ya nchi kupata uhuru.